Baada ya kukabiliwa na scandal kubwa ya kupanga njama za kumuua Ali Kiba, Khalid Mohamed aka Top in Dar, amezungumza na kusema Ali Kiba na mama yake wamekosa la kufanya na anawaona wajinga wakubwa.
Akizungumza
kwenye kipindi cha Tagz Weekly cha DTV, msanii huyo amesema huenda Ali
Kiba alienda kwa mganga ambaye alimwambia TID anataka kumuua.
Msanii
huyo wa ‘Nyota Yangu’ aliongeza kuwa kutokana na kusingiziwa kitu
asichokijua, kamwe haiwezi ikatokea siku atampigia tena simu Ali Kiba
aliyekuwa mshikaji wake wa karibu.
“Siwezi
naogopa,” alisema. “Naweza kumpigia simu nikaambiwa sasa ndo
natamtafuta kumuua, achana naye tu mwache yeye aendelee na vitu vyake,
because I felt he and his family were up to it, mama yake namuona sana,
najua mama yake hanijui hajawahi kuniona hata siku moja.
Ali
Kiba kwa kitu gani ambacho amefanya yeye mimi nimfanyie baya? Nipo na
watu kibao pale nao wamejilist eti nataka kuwaua sasa mimi hela ngapi
nitatoa kuwaua watu wote wale? For what purpose watu kibao wamejilist.
Am
not gonna tell you what reactions I’m gonna do, I’m keeping it to
myself, I aint gonna talk about it, seriously they are stupid, yaani
they should come up with the best concept.”
No comments:
Post a Comment