Friday, August 31, 2012

HUYU NDIE MCHUNGAJI MWENYE UMRI MDOGO DUNIANI, ANA MIAKA 13 TU.

 


Mamake Ezekiel na babake wa kambo ni wachungaji wa kanisa la 'Fullness of time' huko Maryland kanisa ambalo walilianza miaka mbili iliyopita.Ni katika kanisa hili ambapo hezekaiah alitawazwa kuwa mchungaji na ndugu yake shemasi mapema mwaka huu.
'Ulikuwa wakati wa ajabu kwangu' alisema Hezekiah nduguye Ezekiel mwenye umri wa miaka 13.'Kila mtu kanisani alitupigia makofi kwa furaha na kutupongeza'
Micah, nduguye Hezekiah ana mumri wa miaka saba na tayari anataka kufuata nyayo zake hezekaih 'Tayari nimetayarisha mahubiri lakini nitayahubiri nitakapo hitimu miaka 10' alisema Micah kwa sauti ya unyenyekevu.
Sio nchi ya marekani tu ambayo ina watoto wanaohubiri, bali Brazil pia imeboboea katika jambo hili.Indonesia pia haijawachwa nyuma kwani ina kipindi cha runinga ambacho wahubiri wachanga wa dini ya kiislamu hishindana. ini se
'Jambo hili lina uwezo wa kuchipuka haswa katika dini ambazo husisistiza uwepo ya roho mtakatifu na pia jamii zilizotengwa' asema Edith Blumhofer mtaalam wa historia ya wakristo chuo cha Wheaten mjini Illinois.
Ted Lavigne kasisi aliye staafu na anaandika kitabu kilicho na mada hii ya watoto wahuburi,asema kuwa wahubiri wengi watoto walisikika sana miaka ya 1920 na 1930 wakati ambapo kanisa la pentekoste lilikuwa changa.

Fasihi za awali zinaelezea wakati huu ambapo watoto walisikika wakinena maneno yenye hekima kuliko miaka yao.Jambo hili lilipokelewa kwani lilikuwa thibitisho la uwepo wa Roho Mtakatifu.
Jambo la kushangaza ni kwamba,jinsi makanisa haya yalipoendelea kuwatumia watotohawa ndivyo waliendelea kuonekana wamejitenga.

Lavigne amegundua takriban mifano 500 tangu miaka ya 1500 na 1700 ya watoto hawa,wengi wao wakiwa na asili ya marekani na wengine uingereza.

'Kuna elimu ya nguvu ya kidini inayoendelea hapa nchini.Hapa Amerika kuna watu wanaopeda dini sana' asem Randall Balmer mwenyekiti wa kitengo cha dini chuo cha Dartmouth.
Waumini kanisani

Kanuni zinazosema nani anayeweza kuanzisha kanisa zina posho kubwa kwa hivyo mtu yeyote anaweza kuanzisha kanisa mahali popote.Kanisa la familia ya Ezekiel ni kanisa ambalo halifuati madhehebu yoyote kwa hivyo wana uhuru wa kufanya mambo yao vyovyote.
Hata hiyo si vigumu kupata watu walio na wasiwasi kuhusu watoto wahubiri.Watu kama hawa huwa na dhana kuwa ni wachanga sana kuapishwa kama kasisi na wana ushahidi wa kesi za watoto wahubiri waliopotoka.
Ushahidi mkubwa haswa ni ule wa Marjoe Gortner,mtoto mhubiri aliyetangaza baada ya miaka mingi kuwa hakuamini kuwa kuna Mungu na alikuwa mhubiri kwa shinikizo ya wazazi wake na baadaye kama ajira.
Wazazi wa Ezekiel wanafahamu fika mambo haya na wako tayari kumtetea mtoto wao.Mamake asema kuwa watoto wake wana adabu na tabia nzuri.Maisha ya watoto wao ina uwianao,kwani hata ingawa ni wahubiri wao kufanya vitu ambavyo watoto wa kawaida hufanya kama kwenda shule,kucheza na watoto wengine na kadhalika.

Thursday, August 30, 2012

WANACHUO 51 WA UDSM WAACHIWA HURU NA MAHAKAMA.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam imewaachia huru wanafunzi 51 wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) waliokuwa wakikabiliwa kwa pamoja na mashitaka ya kufanya mkusanyiko usio halali tarehe Novemba 11 mwaka 2011, eneo la Mlimani la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kusababisha uvunjifu wa amani eneo la chuo hicho.

Wanafunzi hao waliachiwa jana na Hakimu Walialwande Lema aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo baada ya upande wa mashitaka ulioongozwa na Wakili wa Serikali, Ladslaus  Komanya kushindwa kuleta mashahidi mahakamani huku wakitoa sababu mbalimbali. Komanya alidai kuwa  washtakiwa hao wakiwa kwenye mkusanyiko huo haramu kwa lengo la kufanya mgomo, askari wa Jeshi la Polisi waliwataka watawanyike, lakini hata hivyo wanafunzi hao walikaidi amri hiyo na kudai kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika.

Hata hivyo washitakiwa hao ambao walifikishwa mahakamani hapo chini ya ulinzi mkali wa jeshi la polisi, walikana mashtaka hayo na waliachiwa huru baada ya kukamilisha masharti ya dhamana ya kuwa na mdhamini mmoja wa kuaminika ambaye alisaini bondi ya Shilingi milioni moja.

Baada ya kuachwa huru, wanafunzi hao waliondoka mahakamani hapo kwa furaha huku wakikumbatiana na wengine wakisali.

Akitoa uamuzi huo jana, Hakimu Lema alisema kuwa anatupilia mbali maombi ya upande wa mashitaka yaliyokuwa yakiomba ahirisho la kesi hiyo kwa mara nyingine wakidai kuwa mashahidi wao ambao ni askari wako katika Sensa ya Watu na Makazi.

Lema alisema kuwa sensa ni muhimu kama ilivyo kesi hiyo, lakini maombi yao hayakufuata taratibu za sheria ambapo kwa mujibu wa kifungu cha sheria cha 225 (4) Sheria ya  Mwenendo wa Mashauri ya Jinai (CPA), sura ya 20 kwa sababu upande wa mashtaka ulishindwa kuliendesha shtaka hilo.

“Agosti 13 mwaka huu kulikuwa na ahirisho ambapo sababu ilikuwa hakuna mashahidi kwa sababu wako katika mgomo wa madaktari, leo tena mnaleta sababu kuwa wako katika sensa inaonesha mmedharau amri ya Mahakama,” alisema Hakimu.

Alisema amri ya mwisho aliyoitoa ilikuwa ahirisho la Agosti 13 mwaka huu hivyo upande wa mashitaka umedharau amri ya Mahakama na kwa maana hiyo anawaachia huru washitakiwa wote chini ya kifungu cha sheria ya Mwenendo wa makosa ya jinai kifungu cha 225 (5) sura ya 20.

Awali wakili wa upande wa mashitaka, Prosper Mwangamila alidai kuwa kesi ilikuja kwa ajili ya kusikilizwa akaomba iahirishwe hadi Jumatatu. Wakili wa washitakiwa hao, Reginard Martin akijibu hoja hiyo aliiomba Mahakama kutokubali ombi hilo na badala yake kesi ifutwe washitakiwa waachiwe huru.

Baadhi ya majina ya wanafunzi walioachwa huru ni Mwambapa Elias, Evarist Ambrose, Baraka Monas, Hellen Moshi, Alphonce Lusako, Matrona Babu, Rolanda Wilfred, Godfrey Deogratius, Moris Denis and Evon Gumbi.Others are Lugiko Mathias, Ndimbo Jabir, Evarist Wilson, Cornel Rwaga Mushi, Mlazi Kumbuka, Rehema Munuo, Glory Masawe, Happy Amulike, Elias Mpangala, Frida Timothy, Stella Mofe, Betwel Martin, Mmasi Stephen na Lugemalila Venance na wengineo.

Source:  Habarileo

MAJINA YA VITUO VYA "KUCHIMBA DAWA" HAYA HAPA.

Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) ilifanya kikao na wasafirishaji na kuweka mikakati ya utekelezaji wa agizo la Waziri wa Uchukuzi, Dkt. Harrison Mwakyembe katika Mkutano wa Nane wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 2012 uliomalizika hivi karibuni mjini Dodoma, alipotangaza kukataza tabia ya abiria ya kushuka maporini na kujisaidia ‘kuchimba dawa’ ifikapo leo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyopo kwenye tangazo la SUMATRA kwa vyombo vya habari, itawalazimu abiria kuwa na kiasi cha fedha cha ziada kwa ajili ya kulipia huduma ya maliwato. Hata hivyo, taarifa hiyo haikusema lolote kuhusu watoto na wale ambao wana matatizo ya kupata haja ndogo kila baada ya muda mfupi.

Kwa mujibu wa tangazo la SUMATRA vituo vilivyoainishwa katika barabara kuu tano ni:

Dar es Salaam - Mbeya 

Vituo vilivyoainishwa ni mikoa ya Pwani, Morogoro, Iringa na Njombe. Vituo hivyo ni Ruvu iliko hoteli inayotoa huduma hiyo bure, Chalinze kuna hoteli inahudumia kwa Sh 200; stendi kuu ya mabasi ya Msamvu huduma inatolewa kwa Sh 200 na Ruaha Mbuyuni Hoteli ya Al Jazeera inatoa huduma bure. Kitonga, Hoteli ya Confort inahudumia bure, stendi ya Ipogoro malipo ni kati ya Sh 100 na 200, Mafinga abiria watalazimika kulipia kiasi kama hicho na Makambako malipo yatakuwa kati ya Sh 200 na 300.

Dar es Salaam - Mwanza

Magari yanapitia mikoa ya Pwani, Morogoro, Dodoma, Singida, Tabora na Shinyanga, ‘dawa itachimbwa’ Msamvu, Gairo kuna hoteli ambayo inahudumia bure, Badueli umbali wa kilometa tatu kutoka Dodoma mjini pia huduma ni ya bure. Singida mjini iliko stendi ya mabasi huduma hiyo pia itapatikana kwa malipo ya Sh 200, kituo cha mabasi Nzega mjini huduma italipiwa Sh 200 na katika stendi kuu mjini Tabora malipo ni Sh 200 pia. Katika stendi kuu ya mabasi Shinyanga mjini, huduma hiyo italipiwa Sh 200 na kwa waendao Kagera kupitia Kahama huduma itapatikana stendi kuu ya mabasi kwa kati ya Sh 200 na 300 huku Mwanza mjini katika stendi kuu ya mabasi pia huduma italipiwa Sh 200. Kwa waendao Kagera baada ya kutoka Kahama, huduma zitapatikana Ushirombo kwa Sh 100 na Sh 500 ambapo pia watapata fursa ya kuoga, Chato Sh 200, Muleba Sh 200 na Bukoba Sh 200. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, kwa abiria watokao Kigoma kabla ya kufika Kahama watahudumiwa Kasulu kwa Sh 200, Kibondo kwa Sh 200 na Runzewe kwa Sh 200 pia.

Dar es Salaam - Tanga

Abiria watahudumiwa katika kituo cha mizani Msata bila gharama yoyote sawa na Segera.

Dar es Salaam - Moshi, Arusha na Manyara

Huduma zitapatikana Korogwe katika hoteli mbili bila malipo na Mombo ambako pia kuna hoteli isiyotoza malipo. Lakini Same, Mwanga, Himo, Moshi Mjini na Boma Ng’ombe, huduma itatolewa kwa Sh 200 na Arusha huduma itapatikana stendi kuu kwa Sh 200 sawa na ilivyo kwa Manyara.

Dar es Salaam-Lindi-Mtwara

Eneo la Nangurukuru kuna hoteli iitwayo StarCom ambayo itatoa huduma bila malipo, ambapo Lindi huduma hiyo haitalipiwa huku Mtwara ikilipiwa Sh 200 ingawa haitoshelezi mahitaji.
 

Wednesday, August 29, 2012

OSAMA HAKUULIWA NA MAKOMANDO BALI MAKOMANDO WALIMKUTA KASHAUWAWA.

Osama Bin Laden

Katika kitabu cha "no easy day" kilichoandikwa na mwandishi  MARK OWEN kinachoelezea jinsi operation iliyo ondoa uhai wa Osama Bin Laden ilivyofanyika, kitabu hicho kimeeleza kuwa makomando hao wa Marekani walimkuta Osama akiwa katika dimbwi la damu sekunde chache kabla ya makomando hao kusikia milio ya risasi mbili ikitokea katika chumba ambacho Osama alikutwa ameuwawa, inasemekana alie muua osama hakuoneka kutokana na kutokomea gizani.

Thursday, August 23, 2012

WADADA WATATU JELA KWA KUMBAKA MWANAJESHI




Huko Nigeria wasichana watatu Hannatu Ibrahim [23], Wosila Hassan [20] na Rukayya Hassan [21] wamefikishwa kizimbani baada ya kumbaka mvulana mmoja ambae ni mwanajeshi ajulikanae kwa jina la Abdulrahman Sulaiman,[20].
Ilikuwa ni katika mwezi mtukufu wa Ramadhani katika mji wa Gusau ambapo kijana huyo alipovamiwa na wadada hao watatu alipokuwa anakwenda katika maandalizi ya kujifunza kulenga shabaha, wadada hao walimpeleka mafichoni na kumbaka kijana huyo hadi alipoishiwa nguvu na kuzimia.
Inasemekana sheria ya nigeria haitambui kama ni kosa mwanamke kumbaka mwanaume ila tu mpaka pale atakaposhawishiwa na mwanamke mwenye umri mkumbwa sana zaidi yake.
Kwahiyo mahakama itabidi isubirie upande wa ushaidi kama utasema endapo kijana huyo alipiga kelele za kuomba msaada wakati wa tukio au kama wadada hao walitumia silaha yoyote kumtisha kijana huyo.

Wednesday, August 22, 2012

LL COOL J AMFANYIA KITU MBAYA KIBAKA ALIETAKA KUIBA KATIKA NYUMBA YAKE.


LL Cool J Pic 

Ilikuwa mida ya saa nane za usiku ambapo kibaka mmoja alipovunja na kuingia katika nyumba ya LL COOL J, cool j alishtushwa na alarm ambayo aliiseti katika nyumba yake.
Kwa bahati mbaya mwizi  huyo aliingia choo cha kike kama wasemavyo mtaani, yani alivamia nyumba ambayo hakutakiwa kuingia kwani alipata kipigo kizito kutoka kwa jibaba LL COOL J.
COOL J alimbana kibaka huyo na kuwapigia simu polisi, na baada ya polisi kufika kazi yao ilikuwa ni kumbeba tu mwizi huyo na kumpeleka kituoni.

WAISLAM WAAMUA KUWALINDA WAKRISTO NA MAKANISA HUKO KENYA

 

Viongozi wa kiisilamu nchini Kenya wamekubaliana kuunda makundi ya kutoa ulinzi kulinda makanisa kutokana na mashambulizi kama yaliyotokea kaskazini mwa Kenya siku ya Jumapili.
Watu kumi na tano waliuawa katika mashambulizi mawili dhidi ya makanisa mawili mjini Garissa karibu na mpaka wa Somalia.
Eneo la mpakani mwa Kenya na Somalia limekumbwa na hali ya wasiwasi tangu Kenya ilipopeleka majeshi yake kupambana wanamgambo wa al-Shabab.

Waisilamu wanahisi kuwa kwa sababu wakristo ni wachache katika sehemu hiyo hakuna budi kuwalinda.
"Kuna watu huko nje wanaotaka kufanya kila wawezalo kufanya Kenya kama Nigeria." Alisema bwana Wachu, ambaye pia ni mwenyekiti wa baraza la viongozi wa kidini nchini Kenya."
"Sisi hatutaruhusu kutokea ghasia za kidini nchini humu, yeyote aliye na nia ya kuchochea hali hiyo afahamu kuwa hatafaulu." aliongeza Wachu.
Alisema kuwa sasa ni juu ya viongozi waisilamu mjini Garissa kupanga namna ambavyo makanisa thelathini yaliyo Garissa yatalindwa.
Watu wengi wanaoishi ndani na kando ya mji wa Garissa ni wasomali na ambao ni waisilamu.
Mwezi Oktoba mwaka jana wanajeshi waliingia nchini kupambana dhidi ya al-Shabab wanaotuhumiwa kufanya vitendo kadhaa vya utekaji nyara na kutatanisha usalama kwenye eneo la mpakani.
Lakini tangu hapo Al Shabaab limelaumiwa kwa kufanya msururu wa mashambulizi ya maguruneti katika baadhi ya sehemu za nchi hiyo.
Viongozi wa kundi hilo, hawajajibu shutuma zozote za kufanya mashambulizi ya Garissa.

Tuesday, August 21, 2012

RAIS WA LIBERIA AMSIMAMISHA KAZI MWANAE

Ellen Johnson Sirleaf anashutumiwa kwa kuendeleza upendeleo wa kindugu  

Rais wa Liberia Ellen Johnson Sirleaf, amemsimamisha kazi mmoja wa watoto wake wa kiume kutoka ngazi ya unaibu gavana wa benki kuu ya nchi hiyo kwa kushindwa kuorodhesha mali zake katika tume ya kuzuia rushwa nchini humo.
Charles Sirleaf, ni miongoni mwa maafisa 46 waliosimamishwa kazi kwa kosa hilo.
Ni mmoja wa watoto wake watatu wa kiume aliowateua kushika vyeo vya juu kabisa baada ya kushinda muhula wa pili wa uchaguzi mwaka jana.
Wapinzani wa Bi Sirleaf wanamshutumu kwa kuendeleza upendeleo wa kindugu.
Rais huyo amemteua mtoto wake wa kiume Fumba kuwa mkuu idara ya usalama wa taifa, na kijana mwingine Robert kuwa mshauri mkuu na mwenyekiti wa kampuni ya mafuta inayomilikiwa na serikali-NOCAL.

Thursday, August 9, 2012

MITAMBO YA KUKAMATA CD FEKI YAKAMATWA

 

Mkurungezi wa kampuni ya MSAMA PROMOTION ,Bwa.Alex Msama pichani mwenye fulana ya mistari akiwaonesha waandishi wa habari Cds za video na Audio za Muziki wa aina mbalimbali pamoja na Kompyuta za kudurufu kazi za wasanii kwa njia ya wizi kwenye  kituo kikuu cha Polisi mkoani Dodoma.

Jeshi la Polisi mkoani Dodoma limeendesha Operesheni maalum ya kukamata maharamia wa kazi za wasanii nchini na kufanikiwa kuwatia mbaroni watuhumiwa 25 wakiwa na mashine za kurudufu CD na mali zingine zenye thamani ya zaidi ya Milioni 67.
 
Kufanyika kwa Opresheni hiyo kunafutia taarifa zilizotolewa na baadhi ya wasanii nchini ikiwemo wa filamu, nyimbo za injili na Bongo fleva kulalamikia kitendo cha baadhi ya wenye maduka ya CD mjini Dodoma kuuza kazi zisizokuwa na hatimiliki zao.
 
Akizungumzia tukio hilo, Mkurugenzi wa Msama Auction Mart, ALEX MSAMA amesema vitendo hivyo vinarudisha nyumba maendeleo ya wasanii  kwani licha ya gharama kubwa wanazotumia wamekuwa hawanufaiki na kazi zao.

MAHAKAMA YAMUACHIA HURU BALOZI COSTA MAHALU




MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, leo imemuachia huru Bila hatia aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia Profesa Costa Mahalu na Ofisa Utawala wa ubalozi huo, Grace Martin waliokuwa wakikabiliwa na kesi ya Uhujumu Uchumi na Kuisababishia Serikali hasara ya Euro 2 milioni.
Hukumu hiyo kwa Profesa Mahalu na Martin imetolewa na Hakimu Mfawidhi mkazi wa Mahakama ya Kisutu Mh. Ilivin Mugeta kwa kumuachia huhu mahalu ambaye alikuwa akitetewa na mawakili wakongwe Mabere Marando na wenzake.

Prof. Mahalu alikuwa akikabiliwa na mashtaka sita yakiwamo ya uhujumu uchumi na kuisababishia Serikali hasara ya Euro 2,065,827.60, katika mchakato wa ununuzi wa jengo la Ubalozi wa Tanzania nchini Italia.

Hukumu ya kesi hiyo iliyokuwa ikinguruma mahakamani hapo kwa miaka kadhaa sasa, imefikia tamati leo na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Ilvin Mugeta ambaye amekuwa akiisikiliza.

Awali, hukumu hiyo ilipangwa kusomwa Julai 11, mwaka huu lakini iliahirishwa kutokana na Hakimu Mugeta kukabiliwa na majukumu mengine. Kesi hiyo iliahirishwa na Hakimu Mkazi, Aloyce Katemana na kupanga kuwa hukumu hiyo itasomwa leo.

Kiongozi wa jopo la mawakili wa washtakiwa hao, Mabere Marando alisema jana kwamba anaamini kesi hiyo ambayo imechukua muda mrefu, leo inafikia mwisho kwa Mahakama kutoa hukumu.

Endapo Mahalu na Mwenzake katika makosa kama hayo yaliyokuwa yakiwakabili wangepatikana na hatia adhabu yake ingeweza kuwa kifungo kisichozidi miaka 15 jela.

Kwa mujibu wa Kifungu cha 60 cha Sheria ya Uhujumu Uchumi, Kifungu kidogo cha pili, Mahakama inaweza kutoa amri nyingine ikiwamo mshtakiwa kulipa fidia.

Hukumu ya kesi hiyo leo ilikuwa ikisubiriwa na kwa shauku si tu na Profesa Mahalu na wenzake ambao wangependa kujua hatima yao, bali pia na umma wote wa Watanzania ambao umekuwa ukiifuatilia kwa muda wote kesi hiyo.

Wakati wa utetezi, Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa ambaye ununuzi wa jengo hilo ulifanyika wakati wa uongozi wake, alipanda kizimbani na kumtetea Profesa Mahalu na mwenzake, akidai kuwa mchakato wa ununuzi wa jengo hilo ulifuata sheria.

Mkapa katika ushahidi wake wa utetezi licha ya kudai kuwa mchakato huo ulifuata taratibu na kwamba ni yeye aliyebariki, pia alimmwagia sifa kedekede Profesa Mahalu akidai kuwa ni kiongozi mwadilifu na mwaminifu katika historia yake ya utumishi wa umma.

Akiongozwa na mmoja wa mawakili wanaomtetea Mahalu na mwenzake, Alex Mgongolwa, Mkapa alieleza mchakato wote wa ununuzi wa jengo hilo na malipo yake kwa kuwa lilinunuliwa kwa maagizo ya Serikali yake.

Wakati upande wa mashtaka ukidai kuwapo kwa uhujumu uchumi kutokana na kuwapo kwa mikataba miwili wakati wa ununuzi wa jengo hilo, Mkapa alidai kuwa aliifahamu mikataba yote hiyo na malipo kufanyika kupitia akaunti mbili tofauti.

Alieleza kushangazwa kwake kusikia kuwa aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi wakati huo, Martin Lumbanga katika ushahidi wake alidai kuwa hakujua mchakato wa ununuzi wa jengo hilo, akisema hajui ni kwa nini Lumbanga alisema hivyo.

Mbali na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ambayo wakati wa ununuzi wa jengo hilo, Rais Jakaya Kikwete ndiye aliyekuwa waziri wake, Mkapa alisema wizara nyingine zilizohusika ni Ujenzi na ile ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Alidai kuwa wizara zote hizo zilituma wataalamu wake kwenda kufanya tathmini ya thamani ya jengo hilo kabla ya ununuzi wake. Alisema taarifa iliyotolewa na Waziri wa Mambo ya Nje wakati huo, Kikwete bungeni juu ya ununuzi wa jengo hilo ni sahihi.

Pamoja na mambo mengine, taarifa hiyo inaeleza kuwa jengo hilo lilinunuliwa kwa Sh.2.9 bilioni na kwamba hati za umiliki wake zilishawasilishwa wizarani na kupelekwa kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

“Maneno hayo ni sahihi. Hayo ndiyo ninayoyajua mimi,” alisema Mkapa na kuongeza kwamba hajawahi kupata malalamiko kutoka Italia kuhusu ukiukwaji wa sheria wakati wa mchakato wa ununuzi wa jengo hilo wala kwa mmiliki akidai kuwa alilipwa pungufu ya makubaliano.

Akijibu swali la Wakili Mgongolwa kama alishapata malalamiko yoyote kutoka kwa CAG kuhusu ununuzi wa jengo hilo, alijibu kuwa hajawahi kupokea malalamiko hayo.

Akijibu swali la Wakili wa Serikali, Ponsiano Lukosi kama aliwahi kuuliza ni kwa nini mwenye jengo alitaka alipwe kupitia mikataba miwili, Mkapa alijibu kuwa hakuuliza kwa kuwa alichokuwa anahitaji ni kupata jengo.

Akijibu swali kwamba kama lengo la mwenye jengo kutaka kulipwa kwa mikataba miwili lilikuwa ni kukwepa kodi ya Serikali ya nchi yake, Mkapa alijibu: “Hilo ni tatizo lake na nchi yake, mimi nilikuwa nataka nyumba na nimepata nyumba, nasema Alhamdulillah.”

Pia Mkapa alisema anamshangaa wakili wa Serikali kudai kuwa pesa hizo kulipwa kwa awamu mbili kunaonyesha kwamba Profesa Mahalu alikuwa na lengo za kuzichukua na kuzitumia kwa masilahi yake... “Mimi nitashangaa sana kusikia hivyo na hasa nitakushangaa wewe maana Profesa (Mahalu) mimi namwamini.”

Utetezi wa Profesa Mahalu
Katika utetezi wake, Profesa Mahalu alikana mashtaka hayo na kudai kuwa alipofika katika ubalozi huo alikuta ofisi hizo zikiwa na hali mbaya hali iliyosababisha kutoa fedha zake za mfukoni na kununua samani zenye hadhi ya ofisi ya ubalozi.

Alisema aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Kikwete pia alifika katika ofisi za ubalozi huo na kushuhudia hali hiyo mbaya na kwamba aliunga mkono hoja yake kwamba ofisi hiyo ni mbovu na akashauri ipatikane ofisi yenye hadhi ya ubalozi.

Alisema mwanzoni mwa Juni, 2001 Katibu Mkuu wa Wizara hiyo alimpigia simu akimpongeza kwamba maombi ya wizara yao katika bajeti ya kutaka kila ofisi ya ubalozi inunue jengo lake itapitishwa na Bunge.

Alidai kuwa Katibu Mkuu alimtaka yeye na maofisa wengine wa ubalozi kuanza kutafuta majengo. Alisema baada ya hapo aliwaagiza maofisa wake kwenda kutafuta majengo ndani na nje ya Jiji la Rome kwa ajili ya kulinunua.

Martin katika utetezi wake alidai kuwa, Balozi Mahalu hakuisababishia Serikali hasara ya Euro 2 milioni, bali alileta faida kwa taifa kwa kuwa na jengo zuri na kwamba anahitaji kupewa shukrani.

Akiongozwa na Wakili Marando kujitetea dhidi ya tuhuma zinazomkabili, Grace alidai: “Mheshimiwa kwa ufahamu wangu, Balozi Mahalu mashtaka yote sita yanayomkabili hakuyatenda, aliwasilisha mikataba miwili kama taarifa iliyofanyika kihalali.”

Pia Martin alihoji sababu ya upande wa Jamhuri kutomleta mmiliki wa jengo hilo la ubalozi kukana risiti hiyo au Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hosea kuulizwa juu ya ununuzi wa jengo hilo akidai walikwenda nchini humo kufanya uchunguzi.

Balozi Profesa Mahalu akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kushinda kesi yake katika mahakama ya kisutu leo.