Friday, October 26, 2012
MADEE A.K.A RAIS WA MANZESE AJITOA TIPTOP CONNECTION
hiri wa muziki wa kizazi kipya anayewakilisha pande za Manzese, Hamad Ally ‘Madee’, kutoka kundi la Tip Top Connection, inadaiwa kuwa amejitoa katika kundi hilo, na sasa anataka kufanya muziki kivyake na sababu za kujitoa kwake bado hazijulikana.
Chanzo chetu cha habari kilichozungumza nasi, kwa sharti la kutotajwa kwa jina lake kilidai kuwa wiki iliyopita msanii huyo alikuwa kwenye mzozo na mmoja wa wasanii wa kundi hilo lakini waliweza kupatana ingawa jamaa bado anaonekana kutopenda kile kilichotokea lakini bado kuna vitu vingine vya ndani zaidi vilivyosabisha hadi jamaa kuamua kujiweka pembeni.
Chanzo hicho kilichopo karibu na wasanii hao hakikusita kueleza kuwa ndani ya kundi hilo kuna matatizo mengi, kwani hata kuondoka kwa baadhi ya wasanii waliokuwa hapo kulisababishwa na matatizo hayo ambayo yamemfanya Rais huyo manzese kujiengua, ingawa bado kuna mvutano mkubwa unaoendelea ili kumrudisha kundini jamaa huyo bila taarifa za mkwaruzano huo kutoka nje.
Thursday, October 18, 2012
BIASHARA YA KUUZA BINADAMU(WATOTO WA KIKE) YASHAMIRI ULAYA.
Kumekua na tabia ya kusafirishwa kwa mabinti kutoka nchi mbali mbali kuingia Wingereza,
Idadi hiyo ya mabinti hao sasa imefikia hadi 946 kwa mwaka na kati ya hao 234 ni watoto wadogo.
Mabinti hao wengi hudanganywa kuwa wanaenda kufanya kazi nzuri au kusoma na badala yake hulazimishwa kujiingiza katika biashara za uchangudoa ama kufanywa kama watumwa na kufanyishwa kazi viwandani na mashambani.
Wengi wa mabinti hao huchukuliwa kutoka Romania,Vietnam, China na Nigeria.
Saturday, October 13, 2012
KAMANDA MKUU WA POLISI MWANZA LIBERATUS BARLOW APIGWA RISASI NA KUFARIKI
Mkuu wa jeshi la polisi (IGP) Said Mwema amethibitisha kuuwawa kwa kakamnda wa Mwanza Liberatus Barlow .
Amesema kuwa kamanda huyo wa polisi ameuwawa na watu wanaosadikika kuwa ni majambazi majira ya saa 7.30 na saa 8 usiku katika maeneo ya Kitangiri jijini Mwanza.
Mwema amesema kuwa kamanda Barlow alikuwa akitokea katika kikao cha harusi akiwa njiani kumrudisha dadake nyumbani kwake ghafla alikutwa na tukio hilo la kupigwa risasi.
Hata hivyo alisema kuwa kutokana na tukio hilo jeshi la polisi linataraji kuanza uchunguzi wake kuanzia leo na timu ya askari kutoka makao makuu ya polisi wataondoka mapema leo kwenda jijini Mwanza kuungana na askari wa mkoa huo kwa ajili ya uchunguzi zaidi na msako wa majambazi hayo .
Mwema amewataka wananchi wa Mwanza kutoa ushirikiano wao kwa jeshi la polisi ili kufanikisha zoezi hilo na kuwataka kutokuwa na hofu yoyote kutokana na tukio hilo.
NAKAAYA SUMARI AZIANIKA NYETI ZAKE HADHARANI
Imekuwa kitu cha kawaida sana kwa siku za hivi karibuni kwa wadada maarufu kuanika makufuli yao pamoja na nyeti zao hadharani,na huyo hapo juu ni Nakaaya Sumari na jambo la kusikitisha hata kufuli hajavaa(nguo ya ndani).
Friday, October 12, 2012
AJIRA KWA WATOTO ZITAISHA LINI?
Watoto wakazi wa kata ya Sinde Mtaa wa Kijani Bichi, Ilolo mkoani Mbeya wakitumikishwa kubeba matofali kwa ujira wa shilingi 10 kwa tofali pamoja na jitihada za kukomesha ajira za watoto lakini bado tabia hiyo imekuwa ikiendela katika maeneo mengi nchini
Tuesday, October 2, 2012
MWANAFUNZI BRAZILL AWEKA BIKRA YAKE MNADANI ILI KUPATA FEDHA ZA KUJENGA NYUMBA ZA WATU MASIKINI.
Huyu ndie msichana wa miaka 20 wa Kibrazill ambae pia ni mwanzafunzi wa chuo, mrembo huyu ameamua kuifanyia mnada bikra yake na kwa mtu atakae toa dau kubwa ndie atakae mtoa bikra, hela hiyo itakayopatikana itasaidia kujenga makazi ya watu masikini katika mji wake wa jimbo la Santa Catarina kusini mwa brazill.
Zoezi la kutoa bikra hiyo litafanyika ndani ya ndege itakayosafiri kutoka Australia hadi Marekani, na mshindi atapimwa magojwa yote ya zinaa na condom itatumika ili kuepuka sheria zote uchangudoa.
Anaeongoza kwa dau kubwa mpaka sasa ni Mmarekani Jack Mille ambae anaongoza kwa dau la $160,000.
TUME YA MAWASILIANO KENYA YAZIMA SIMU ZOTE ZA KICHINA(FEKI).
Wateja milioni 2.5 wa Simu za
rununu leo wamejipata mashakani baada ya Tume ya Mawasiliano nchini
Kenya kuzima simu ghushi.
Zoezi hilo la kuzima simu lilianza kutekelezwa
usiku wa manane na linalenga kukabiliana na uingizaji wa simu bandia,
suala linalohujumu juhudi za kuimarisha usalama.Hatua ya kuzima simu ghushi na ambayo imethibitishwa na kampuni nne za huduma za simu nchini humo, inafuatia agizo la tume ya wasiliano nchini humo ambayo inataka kukabiliana na biashara haramu, wizi wa haki miliki na tisho la usalama.
Afisaa mkuu mtendaji wa tume hiyo, Francis Wangusi, alielezea kuwa hatua ya kuzima simu hizo, ambayo ilikuwa imeakhirishwa mara tatu iliweza kutekelezwa usiku wa kuamkia leo.
Tume hiyo haijashirikiana na kampuni za huduma za simu kuzima simu ghushi tu bali pia simu ambazo wateja wake hawajasajiliwa.
Hatua hii imesababisha hasare kubwa kwa kampuni za simu.
Hata hivyo tume ya CCK, imetenga bajeti ya pesa itakazotumia kugharamia hasara ya kampuni za simu ingawa wateja wa simu hizo hawatapata fidia yoyote.
Kampuni ya Safaricom, ambayo ina wateja wengi zaidi ya kampuni zote za huduma za simu za rununu nchini Kenya, imezima simughushi, 670,000 katika masaa 15 pekee.
Kampuni ya Airtel Kenya nayo imezima simu 100,000 huku yuMobile ikizima takriban simu 45,000. Kampuni ya Telkom Orange imezima takriban simu 20,000.
Nani wa kulaumiwa kwa kuingiza nchini simu bandia?
MUME WA MTU ANAETAFUTA WANAWAKE facebook WA KUWALA TIGO(KUMWINGILIA MWANAMKE KINYUME NA MAUMBILE) NI HUYU.
Mpendwa msomaji, huyu ni Nancy Mitikisiko aliyekumbwa na zali la kuombwa Tigo......
Jambo hilo lilimkera, lakini braza huyo aling'ang'ania apewe au atafutiwe......
Varangati lilienda mbali zaidi mpaka wakaanza kupeana matusi ya nguoni.
Halafu Yakaendelea Hivi....
CHANZO :
NANCY MITIKISIKO SALAMBA,
RAHATUPU BLOG,
rahatupu.blogspot.com.Monday, October 1, 2012
LINAH:BABA HATAKI KUNIELEWA KISA MAVAZI YANGU YA NUSU UCHI, NAMI SIWEZI KUVAA MAGAUNI KAMA NIPO KANISANI.
Mwimbaji Linah ambae juzi alitangaza kwamba ameamua kuwazawadia wazazi wake nyumba aliyoijenga Mpiji Mbezi Dar es salaam kwa thamani ya milioni 30 za kitanzania, amesema pamoja na wazazi wake kufahamu kwamba matunda hayo yametokana na muziki peke yake, amekubali kwamba baba yake mzazi mpaka sasa bado hakubaliani na mavazi anayoyavaa Linah.
Namkariri Linah akisema “nimejitahidi sana kuwaelezea wazazi wangu wanielewe litakapotokea tatizo lolote itakua ni bahati mbaya tu lakini sio kwa makusudi, baba anaona pia kwenye magazeti huwa navaa hivi najitahidi kumwambia hivyo ni vitu vya bahati mbaya huwa vinatokea na mimi kama msanii ndio maana tunakula tunaishi lakini ndio kazi”
Mbali na hayo Linah kasema
“nyimbo zangu baba anazisikiliza na anazipenda na anakubali ninaimba
kitu ambacho kipo, ila ubishi mkubwa kati yangu na yeye ni mavazi, kuna
show na show.. siwezi kwenda kufanya show ufukweni alafu nimevaa
magauni, show nyingine tunatakiwa kubang siwezi kuvaa migauni kama niko
kanisani”
Subscribe to:
Posts (Atom)