DIVA ANASEMA:
Kuna kitu kimoja nakiogopa sana katika maisha nacho ni kuzaa
mtoto. naogopa sana sana kuzaa mtoto ,Process nzima ya kuwa na mimba
yaani tumbo kuwa kubwa kwanza naogopa na naona aibu sana yaani nahisi
kwanza nikiwa na tumbo kubwa kabisa la mimba ntakuwa najifungia ndani na
sitatoka kabisa mtu anione kitu ambacho kitakuwa kigumu coz its a
hustler , kabisa !!Na naogopa yale maumivu wakati unazaa .. nikiangaliaga movie huwa nalia na nazima tv na kuondoka kabisa eneo hilo naogopa sana kuzaa mtoto ,naogopa pia mama mjamzito huwa natetemeka nikiona mtu ana mimba sana sijaelewa kwanini ila hilo ndilo jambo naogopa sana.
sitaki hata anisogelee , nakumbuka mtu mmoja tu kumshika tumbo lake alikuwa zamaradi mketema nikamuuliza haliumi akasema haliumi , iko siku na wewe utatamani tu , sasa hivi unasema tu. ila wakati namshika tumbo nilikuwa naogopa natetemeka, huyo ndo mtu wa pekee niliewahi kumgusa tumbo la mimba , sirudii tena yaani maana nilihisi kama namuumiza.
No comments:
Post a Comment