Wednesday, June 27, 2012
AMITABH BACHCHAN HAJAFA
Kumekuwa na habari zikiendelea midomoni mwa watu kuwa Star wa Bollywood Amitabh Bachchan amefariki kwa ajari ya gari.
Mtandao wa THE TIMES OF INDIA umethibitisha kuwa Amitabh hajafa na stori za kifo chake zilianzia katika blog moja iliyoweka hadi picha ya ajari ya gari aliyopata star huyo.
kumekuwa kukizushwa habari za uwongo hivi karibuni, kwani hivi karibuni star mwingine wa Bollywood RAJESH KHANNA alizushiwa amefariki .
Amitabh yupo hai na anaendelea ku tweet katika mtandao wa twitter ingawa hajasema chochote kuhusu uzushi huo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment